Thursday, December 31, 2009
Saturday, December 26, 2009
Tuesday, December 8, 2009
Monday, November 30, 2009
KAMPUNI YA KINGUNGE YAJITETE JUU YA TAMKO LA JIJI LA DAR ES SALAAM
UONGOZI wa Kampuni ya Smart Holding ya familia ya mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru, imeibuka na kujitetea kwamba, upungufu wa mapato uliojitokeza wakati wa ukusanyaji mapato kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), ulitokana na sababu mbalimbali, zikiwemo za kutotoza ushuru baadhi ya maeneo ndani ya kituo hicho.
Utetezi huo wa kampuni hiyo, unakuja kipindi ambacho tayari jiji limetengua kazi hiyo kwa kampuni hiyo huku ikitangaza kuongezeka mapato muda mfupi baada ya halmashauri kusimamia ukusanyaji wake.
Akizungmza na Mwananchi jijini Dares Salaam juzi, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Hassani Khan, alisema jiji wasijidangnye kwa kipato wanachokipata kwa sasa kwani ni msimu tu.
Alifafanua kwamba, kupata kipato hicho kunatokana na halmashauri kuongeza wigo wa maeneo ya kukusanya kodi.
“Sisi tulipoingia mkataba na jiji wa kukusanya mapato katika kituo hicho, walituwekea mipaka yamaeneo ya kukusanya mapato na kwingine wakikusanya wenyewe jiji,’alitoa utetezi huo.
“Sehemu kama Hotel iliyopo ndani ya kituo na baadhi ya ofisi ambazo si vizuri kuzitaja na zilikuwa na mapato makubwa kutokana na umiliki wao wa sehemu karo husika, walikusanya wenyewe jiji,”aliongeza Khan.
Khani alisema kipato hicho ni kidogo tu kwa jiji kwani , wao walikuwa wakipata Sh 67 milioni, ambazo zilikuwa zinapatikana getini kwa mwezi tofauti na sehemu nyingine ukilinganisha na ukubwa wa kituo.
Alisema hali katika kituo hicho ilibadilika baada ya jiji kubanwa juu ya mapato ya kituo, wakati wa ziara yake mwanzoni mwa mwaka huu ambapo Waziri Mkuu aliagiza kufanyika kwa uchunguzi wa hesabu za uendeshaji.
Baadaye matokeo ya ukaguzi huo uliofanywa na ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kukiwa na taarifa ya kuwepo kwa ubadhirifu na baadaye taarifa zaidi zikibaisha kuondolewa kwa kampuni hiyo kuendesha kituo hicho.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alisema katika muda wote wa miaka mitano waliokuwa wakiendesha makusanyo ya ushuru walikuwa wakipata kati ya Sh1.8milioni hadi Sh 2milioni kwa siku.
Makusanyo hayo yalikuwa ni ushuru wa magari, wasindikizaji na wapokeaji wageni ambapo halmashauri ya jiji ilikuwa ikichukua Sh 1.5milioni bila ya kukosa ambazo ni asilimia 75 na kampuni yake kupata asilima 25.
Alisema mwaka 2004 ,Wizara ya fedha iliteua kampuni binafsi ya CMK ili ifanye tathimini ya kimahesabu kujua kiasi cha mapato yanayotokana na ukusanyaji wa milango pekee yanayoweza kufikia Sh 1.8milioni.
Wakati huo huo Khan alifafanua kwamba kampuni yake haijapata barua yoyote kutoka jiji juu ya kupata kazi ya ukusanyaji mapato kwenye majengo Machinga Complex.
Utetezi huo wa kampuni hiyo, unakuja kipindi ambacho tayari jiji limetengua kazi hiyo kwa kampuni hiyo huku ikitangaza kuongezeka mapato muda mfupi baada ya halmashauri kusimamia ukusanyaji wake.
Akizungmza na Mwananchi jijini Dares Salaam juzi, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Hassani Khan, alisema jiji wasijidangnye kwa kipato wanachokipata kwa sasa kwani ni msimu tu.
Alifafanua kwamba, kupata kipato hicho kunatokana na halmashauri kuongeza wigo wa maeneo ya kukusanya kodi.
“Sisi tulipoingia mkataba na jiji wa kukusanya mapato katika kituo hicho, walituwekea mipaka yamaeneo ya kukusanya mapato na kwingine wakikusanya wenyewe jiji,’alitoa utetezi huo.
“Sehemu kama Hotel iliyopo ndani ya kituo na baadhi ya ofisi ambazo si vizuri kuzitaja na zilikuwa na mapato makubwa kutokana na umiliki wao wa sehemu karo husika, walikusanya wenyewe jiji,”aliongeza Khan.
Khani alisema kipato hicho ni kidogo tu kwa jiji kwani , wao walikuwa wakipata Sh 67 milioni, ambazo zilikuwa zinapatikana getini kwa mwezi tofauti na sehemu nyingine ukilinganisha na ukubwa wa kituo.
Alisema hali katika kituo hicho ilibadilika baada ya jiji kubanwa juu ya mapato ya kituo, wakati wa ziara yake mwanzoni mwa mwaka huu ambapo Waziri Mkuu aliagiza kufanyika kwa uchunguzi wa hesabu za uendeshaji.
Baadaye matokeo ya ukaguzi huo uliofanywa na ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kukiwa na taarifa ya kuwepo kwa ubadhirifu na baadaye taarifa zaidi zikibaisha kuondolewa kwa kampuni hiyo kuendesha kituo hicho.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alisema katika muda wote wa miaka mitano waliokuwa wakiendesha makusanyo ya ushuru walikuwa wakipata kati ya Sh1.8milioni hadi Sh 2milioni kwa siku.
Makusanyo hayo yalikuwa ni ushuru wa magari, wasindikizaji na wapokeaji wageni ambapo halmashauri ya jiji ilikuwa ikichukua Sh 1.5milioni bila ya kukosa ambazo ni asilimia 75 na kampuni yake kupata asilima 25.
Alisema mwaka 2004 ,Wizara ya fedha iliteua kampuni binafsi ya CMK ili ifanye tathimini ya kimahesabu kujua kiasi cha mapato yanayotokana na ukusanyaji wa milango pekee yanayoweza kufikia Sh 1.8milioni.
Wakati huo huo Khan alifafanua kwamba kampuni yake haijapata barua yoyote kutoka jiji juu ya kupata kazi ya ukusanyaji mapato kwenye majengo Machinga Complex.
Mrema atangaza kumvaa Kimaro Vunjo
BAADA ya kushindwa kufua dafu mara tatu katika mbio za urais, hatimaye mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustino Mrema amerejea kwenye kinyang'anyiro cha ubunge baada ya kutangaza kuwa atapambana na Aloyce Kimaro kuwania jimbo la Vunjo.
Mrema, ambaye amewahi kugombea urais akiwa na NCCR Mageuzi na baadaye TLP, alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 20 kabla ya kutofautiana na serikali na baadaye kujiunga na upinzani katika miaka ya tisini.
Wakati hali ikionekana kumuendea kombo Kimaro kwenye jimbo hilo, Mrema anaonekana kutaka kutumia mwanya huo kurudi Vunjo ambako TLP ina nguvu kubwa.
Mwenyekiti huyo wa TLP aliliambia gazeti hili jana kuwa baada ya kumtikisa Kimaro katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu ambao chama chake kimeshinda katika vijiji 20 na vitongoji 48 dhidi ya vijiji 47 vya CCM, sasa anajipanga kwenda jimboni humo kugombea ubunge mwakani.
"Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa, sasa namtangazia rasmi Kimaro kwamba mwakani naenda Vunjo kulichukua jimbo langu. Kimaro ameshindwa kuwasaidia wananchi ndio maana wamemzomea," alisema Mrema alipoongea na Mwananchi jana.
Mrema, ambaye alikuwa waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya awamu ya pili,
Mrema, ambaye amewahi kugombea urais akiwa na NCCR Mageuzi na baadaye TLP, alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 20 kabla ya kutofautiana na serikali na baadaye kujiunga na upinzani katika miaka ya tisini.
Wakati hali ikionekana kumuendea kombo Kimaro kwenye jimbo hilo, Mrema anaonekana kutaka kutumia mwanya huo kurudi Vunjo ambako TLP ina nguvu kubwa.
Mwenyekiti huyo wa TLP aliliambia gazeti hili jana kuwa baada ya kumtikisa Kimaro katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu ambao chama chake kimeshinda katika vijiji 20 na vitongoji 48 dhidi ya vijiji 47 vya CCM, sasa anajipanga kwenda jimboni humo kugombea ubunge mwakani.
"Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa, sasa namtangazia rasmi Kimaro kwamba mwakani naenda Vunjo kulichukua jimbo langu. Kimaro ameshindwa kuwasaidia wananchi ndio maana wamemzomea," alisema Mrema alipoongea na Mwananchi jana.
Mrema, ambaye alikuwa waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya awamu ya pili,
Thursday, November 19, 2009
Friday, November 13, 2009
Muhimbili waanza mgomo baridi
WAFANYAKAZI wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jana walianza kufanya mgomo baridi ili kuishinikiza Serikali kuwalipa ya nyongeza ya mishahara waliyoahidiwa tangu Julai mwaka huu.
Uamuzi wa wafanyakazi hao kufanya mgomo huo baridi unasababishwa na subira yao ya muda mrefu juu ya madai yao kugonga ukuta huku Serikali ikiendelea kuwapiga danadana.
Hata hivyo, wafanyakazi hao waliafikiana kuwa mgomo huo utaanza rasmi Novemba 28, mwaka huu kama serikali hatatekeleza makubaliano yao.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu (Tughe),tawi la Muhimbili, Nusura Barakabitse alisema mgomo uliopo katika hospitali hiyo hivi sasa ni baridi; ambapo wanafanya kazi kinyume na taratibu zao za kila siku.
Alifafanua kuwa mgomo huo ambao sasa hivi unaoendeshwa kisirisiri utakuwa wa wazi ifikapo Novemba 28, wakati wafanyakazi wanapokea mishahara.
Alifahamisha kuwa wamepanga kuanza tarehe hiyo ili waone kama serikali itakuwa imefanya marekebisho ya mishara yao au la na kwamba, wakirekebishiwa hawatagoma.
Alisema wafanyakzai wanashangaa kuona mwajiri wao ambaye ni serikali ameshinda kutekeleza madai yao ya kuongeza mishahara kwa asilimia nne kuanzia Julai, mwaka huu.
Kiongozi huyo wa chama cha wafanyakazi, alisema wafanyakazi hao wamesubiri kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote huku Serikali ikiendelea na hadithi zake kuwa madai yao yanafanyiwa kazi.
Barakabitse alieleza kuwa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi kuwa wataanza mgomo, uongozi wa Tughe uliamua kuonana na uongozi wa MNH na Hazina, ambao walisema fedha za nyongeza ya mishahara zinaandaliwa.
Alisema suala la kucheleshwa nyongeza ya mshahara ya wafanyakazi wa MNH, lianza baadaya sakata lililoibuliwa na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), kwamba kuna wafanyakazi 364 hewa katika hospitali hiyo ambao hawatambuliki na serikali.
Hata hivyo,alisema uongozi wa Tughe unajiandaa kuonana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kumuelezea juu ya mgomo utakaofanyika Novemba 28, kwamba utakuwa ni mkubwa kutokana na hasira za wafanyakazi, hivyo kusababisha athari kubwa.
Source: Gazeti la Mwananchi
Uamuzi wa wafanyakazi hao kufanya mgomo huo baridi unasababishwa na subira yao ya muda mrefu juu ya madai yao kugonga ukuta huku Serikali ikiendelea kuwapiga danadana.
Hata hivyo, wafanyakazi hao waliafikiana kuwa mgomo huo utaanza rasmi Novemba 28, mwaka huu kama serikali hatatekeleza makubaliano yao.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu (Tughe),tawi la Muhimbili, Nusura Barakabitse alisema mgomo uliopo katika hospitali hiyo hivi sasa ni baridi; ambapo wanafanya kazi kinyume na taratibu zao za kila siku.
Alifafanua kuwa mgomo huo ambao sasa hivi unaoendeshwa kisirisiri utakuwa wa wazi ifikapo Novemba 28, wakati wafanyakazi wanapokea mishahara.
Alifahamisha kuwa wamepanga kuanza tarehe hiyo ili waone kama serikali itakuwa imefanya marekebisho ya mishara yao au la na kwamba, wakirekebishiwa hawatagoma.
Alisema wafanyakzai wanashangaa kuona mwajiri wao ambaye ni serikali ameshinda kutekeleza madai yao ya kuongeza mishahara kwa asilimia nne kuanzia Julai, mwaka huu.
Kiongozi huyo wa chama cha wafanyakazi, alisema wafanyakazi hao wamesubiri kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote huku Serikali ikiendelea na hadithi zake kuwa madai yao yanafanyiwa kazi.
Barakabitse alieleza kuwa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi kuwa wataanza mgomo, uongozi wa Tughe uliamua kuonana na uongozi wa MNH na Hazina, ambao walisema fedha za nyongeza ya mishahara zinaandaliwa.
Alisema suala la kucheleshwa nyongeza ya mshahara ya wafanyakazi wa MNH, lianza baadaya sakata lililoibuliwa na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), kwamba kuna wafanyakazi 364 hewa katika hospitali hiyo ambao hawatambuliki na serikali.
Hata hivyo,alisema uongozi wa Tughe unajiandaa kuonana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kumuelezea juu ya mgomo utakaofanyika Novemba 28, kwamba utakuwa ni mkubwa kutokana na hasira za wafanyakazi, hivyo kusababisha athari kubwa.
Source: Gazeti la Mwananchi
Subscribe to:
Posts (Atom)