Wednesday, February 22, 2012

Mchuano mkali kwa wapiga vinanda ambao utafanyika March 3,DAR LIVE




Marchi mbili mwaka huu,
wapenzi wa muziki wa taarab nchini wanaisubiria kwa hamu hususan wale
wanaoingia katika ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala.
Siku hiyo wapapasa vinanda maarufu akiwemo Mfalme Mzee Yussuf (Jahazi), Ally
Jay (5stars) na Thabit Abdul (Mashauzi Classic) watakapochuana katika mpambano
wa kupapasa vinanda.
Mpapano huo umepangwa kufanyika katika ukumbi huo na kila mtu hivi sasa
anazungumzia mpambano huo.

Wema kuendeleza raha nje ya nchi


MSANII mkali katika tasnia ya maigioz nchini ambae pia ni mlimbwende wa Tanzania mwak 2006 ,Wema Sepetu ameamua kufanya vitu vikali nje ya tanzania baada ya kupata pesa kutokanana na kazi yake ya kuigiza inayozidi kumuuzia jina

Mashujaa band kujinoa na vifaa vipya




KUNDI la Mashujaa Music linatarajia kuingiza kambini
wanenguaji wake kwa ajili ya kujifua mtindo mpya kwa ajili ya kupagawisha
katika maonyesho yao ndani ya kipindi hiki.
Akizungumza na starehe meneja wa bendi hiyo Max
Luhanga anasema lengo la kuingia kambini ni kujipanga katika kuimarisha bendi
na kujiweka sawa.
Anasema katika kuimarisha bendi ikiwa na kujipanga
na kutaka kuonyesha umairi katika jukwaa kulingani na ushindani uliopo kwa
sasa.
“Tumepania kuwa juu katika burudani ndani na nje ya
Dar es Salaam na tumeshapokea vifaa vipya vya muziki na kujifua kufanya
mapya,’anasema Luhanga
Anasema katika kuingia kambini bendi imeweka
mikakati ya kuendeleza kufanya vizuri kama kawaida yake na kuandaa kuafanya
makali zaidi.
MWISHO

TSJ kutoa mmoja Miss Tanzania 2012

CHUO cha uandishi wa habari cha Time School of Journalism(tsj) kinatarajia kutoa mmoja kati ykatika mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2012

Hanifa Maulid kutema cheche Kings Modern taarab

BAADA
ya kutamba katika tasnia ya muziki wa taarabu kundi la Mashauzi Classic limekuwa likiongoza
kwa wasanii wamekuwa wakihama kundi hilo
huku wakinukuliwa mara kwa mara na vyombo kwa kirusha makombora kwa muimbaji
kindawa kundi hilo Isha Ramadhani

Hadi
sasa kundi hilo limeshapoteza wasanii kama Rahma Machupa, Zainab Machupa,
Ashura Machupa na Hanifa Maulid ambao wamehama katika makundi mbalimbali ya
muziki.

Mmoja
kati ya wasanii aliyehamia katika kundi la Kings Modern taarab ambaye kwa
kipindi cha nyuma alikuwa akifanya vizuri katika kundi la Mashauzi ,Hanifa
Maulid anasema ameamua kuondoka Mashauzi Classic kutokana na kukosa uhuru
katika kazi.

Anasema
nimeondoka mashauzi bila kufukuzwa ila nimeondoka na kutokana na kuonekana
kwa makosa katika suala la uimbaji hali
iliyokuwa nikionekana kama nafanya makusudi.

“Nimkali
katika suala la uimbaji lakini kutokanana na masula ya matatizo(stress) niliweza
kuteteleka katika uimbaji kama kutoka nje yakii hali hiyo ikachangia kuonekana
sio mtendaji mzuri wa kazi hali ilivyokuwa ikiniuma sana,lakini ilikuwa si
makusudi ni matatizo tu,’anasema Hanifa

Anasema
baada ya hali hiyo kuendelea katika kundi hilo nilimua kuhamia kundi la Kings,
ili niweze kupunguza malumbano.

Kufuatia
hali hiyo sasa hivi ni muimbaji wa kundi la Kings modern taarabu ambapo kwa
sasa ameshandaanymbo inayotambulika ‘Kash kash za mapenzi’itakayoanza kusikika
mwisho wa mwezi huu.

Anasema
kutokana na kujua umuhimu w kazi yake amewahidi wshabiki wa muziki wa taarabu
kuendelea kuwapa burudani kama kawaida yake.

mwisho

Mashauzi kazini


Wanne wachomoka Mashauzi Classic

Mwandishi
wetu
BAADA
ya wasanii wa muziki kuhama hama katika makundi yao walionza nayo kazi taswira
imebadilika sasa katika kundi la Mashauzi Classic kuonokewa na wasanii wanne,
ambako kila anayeamua kuchomoka, huibua kashfa nzito, hususan kumwelekea Isha
mwenyewe.

Wasanii
hao waliongoka ni Rahma Machupa, Zainab Machupa, Ashura Machupa na Hanifa
Maulid.

Wapo
walioondoka kwa kudai kuwa wamechoshwa na ubinafsi, chuki, majungu na roho
mbaya ndani ya kundi hilo, vinavyotiwa chumvi na Isha mwenyewe, huku wengine
wakisema, wivu wa Isha kwa Thabit Abdul unawaweka katika wakati mgumu.
Wiki
iliyopita nilibahatika kumtazama Isha alipokuwa
Isha
athibitishe shutuma nyingi hizi na zile anazotupiwa na baadhi ya wasanii
wanaohama Mashauzi Classic, ambako alitoa majibu yaliyojaa hekima za hali ya
juu kiasi cha kunipa msukumo wa kumtafuta ili nipate maelezo ya kina kutoka
kwake.
“Unajua,
yote yanayosemwa yanasemwa na watu kama mimi, wenye midomo na uhuru wa kuongea,
kwahiyo inakuwa vigumu kuyazuia,” ndivyo anavyoanza kueleza Isha anayetamba
sasa na kibao ‘Si Bure Una Mapungufu’, baada ya kukutana naye nyumbani kwake,
Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Isha
anasema kuwa, mengi yanayovumishwa kila uchao juu yake yanakosa makali zaidi
kutokana na yeye mwenyewe kuamua kukaa kimya bila kujibu, ambako anadai
usipiomjibu mtu tayari umemwambia anyamaze.

Anasema,
kinachomsikitisha zaidi na zaidi ni kuona kuwa, wote wanaomzushia kashfa na
shutuma hizo ni wale chipukizi ambao.

Kwa
namna hii ama ile, nguvu zake zimetumika ipasavyo kuwafikisha hapo walipo sasa.

Anazidi
kusema kuwa, kwa upande wake anaona kuwa si vema kwa wasanii wanaochipukia
katika muziki kujiingiza katika utamaduni wa kutafuta umaarufu kwa nguvu na
badala yake wajibidiishe jukwaani kupitia vipaji walivyonavyo.
Anasema,
anashangaa kuona kuwa, imekuwa ni desturi kubwa kwa wasanii wengi hapa nchini,
hususan chipukizi wanapotoka kundi moja kwenda jingine, kuanzisha chuki kati
yao na kundi walilohama.
"Binafsi,
naona jitihada ndio silaha nzuri zaidi kwa msanii, kwasababu hata mimi
nilipotoka Jahazi Modern sikuanza malumbano, ingawa wakati mwingine tulikuwa
tukikosana kama ilivyo kwa wengine wote kwenye sekta mbalimbali," anasema
Isha.
Anasema
kuwa, jambo analopaswa kulizingatia msanii ni jinsi atakavyoweza kusimama
jukwaani kuimba na kumudu kuwanyanyua vitini japo mashabiki watano, na si
kutafuta umaarufu kupitia migongano isiyona msingi.
Kuhusiana
na suala la kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Thabit, Isha anasema kuwa
alishakataa mara nyingi na ataendelea kukataa siku zote, huku akiweka wazi kuwa
uhusiano wake na Thabit unaishia kwenye muziki pekee.

Anaeleza
kuwa, Thabit, kati ya wapapasa vinanda mahiri hapa nchini, ni Mkurugenzi
mwenzie ndani ya Mashauzi Classic, ambako pia anamuheshimu akimwita ‘mjomba’
kutokana na kuwa ni mkubwa zaidi kwake, aliyeanza muziki kabla yake.
“Kiukweli,
mtu ukishakuwa maarufu kuna mambo ambayo huwezi kuyaepuka, hivyo kwa upande
wangu, nazipokea kashfa na shutuma zote ninazorushiwa na kuzichukulia kuwa ni
kati ya changamoto muhimu katika maisha ya ustaa,” anasema Isha.

Hata
hivyo, Isha anasema kuwa, yote yanayosemwa kwa nia mbaya kwake, yanampa ari,
kasi pamoja na nguvu ya kujituma na kujibidiisha zaidi jukwaani ili kuhakikisha
kuwa, malengo ya wasiopenda maendeleo yake hayatimii kirahisi.


Kufuatia
hali hiyo sasa hivi ni muimbaji wa kundi la Kings modern taarabu ambapo kwa
sasa ameshandaanymbo inayotambulika ‘Kash kash za mapenzi’itakayoanza kusikika
mwisho wa mwezi huu.
Anasema
kutokana na kujua umuhimu w kazi yake amewahidi wshabiki wa muziki wa taarabu
kuendelea kuwapa burudani kama kawaida yake.
MWISHO

kikosi cha Mizinga live News Maisha Club


Jenipher kutoka na Dhahabu 2012

MWANAMUZIKI wa mziki wa injili nchini Jenipher
Mgend anatarajia kuachaia albamu itakayotamba kwa jina la DHAHABU yenye mkusanyiko wa baadhi ya nyimbo zangu za zamani kama vile
Nini?, Nimrudishie nini Bwana, Nitafika lini?, Mbona washangaa njiani. Ulinipa
sauti na nyinginezo ambazo zilitamba miaka ya 2001 na kurudi nyuma hadi mwaka
1995. Albamu hii tayari ipo madukani katika mfumo wa audio cd yaani ni ya
kusikiliza. Maandalizi ya video hii yanafanyika na panapo manajliwa mwezi
Agosti itakuwa imekamilika.TEKE LA MAMAFilamu hii ipo madukani na
imewashirikisha watu mbalimbali kama Bahati Bukuku, Christina Matai, Senga,
Lucy Komba na Godliver a.k.a Bibi Esta. Sio filamu ya kukosa kuangalia na uzuri
wake unaweza kuiangalia ukiwa umetulia na familia yako bila kuwa na wasiwasi wa
kuanza kuwatuma watoto dukani ili wasione picha chafu.SHEREHE ZA MIAKA 15 YA
HUDUMAPanapo majaliwa na Mungu, natarajia kufanya tamasha la kusherehekea
na kumshukuru Mungu kwa miaka 15 tangu nianze huduma ya uimbaji. Tamasha au
sherehe hiyo inatarajiwa kufanyika tarehe 05 Agosti, 2012 katika ukumbi wa
Landmark Hotel.Video ya album ya Dhahabu itazinduuliwa siku hiyo pia.
Maandalizi ya tamasha hili yanaendelea na litapambwa na waimbaji mbalimbali
watakaoimba live siku hiyo. Sio siku ya kukosa na wote wenye mapenzi mema
wanaombwa kujitokeza kwa wingi. Tutaendelea kuhabarishana kuhusu tukio hili
kadiri siku zinavyoendelea.ALBAM MPYAMaandalizi ya album mpya
yanaendelea moyoni lakini rasmi kabisa yataanza mara baada ya tamasha la mwezi
wa Agosti na album hii mpya inatarajiwa kuingia sokoni mwezi Aprili mwaka 2013,
tukijaliwa uzima.